Kitabu Cha Mistari Ya Bibilia Ya Kukari
3/5
()
About this ebook
Usiku mmoja, wakati akiwa ni mwanafunzi wa utabibu katika mji mmoja huko Ghana, katika hali ya mwujiza Mungu alimpaka mafuta Dag Heward-Mills wakati alipokuwa akimsubiri Bwana. Alipakwa mafuta kwa namna isiyo ya kawaida na kusikia maneno, “Tangu sasa na kuendelea unaweza kufundisha...” Wito huu usio wa kawaida ndio uliomwongoza kwenye huduma iliyosambaa duniani kote.
Dag Heward-Mills
Bishop Dag Heward-Mills is a medical doctor by profession and the founder of the United Denominations Originating from the Lighthouse Group of Churches (UD-OLGC). The UD-OLGC comprises over three thousand churches pastored by seasoned ministers, groomed and trained in-house. Bishop Dag Heward-Mills oversees this charismatic group of denominations, which operates in over 90 different countries in Africa, Asia, Europe, the Caribbean, Australia, and North and South America. With a ministry spanning over thirty years, Dag Heward-Mills has authored several books with bestsellers including ‘The Art of Leadership’, ‘Loyalty and Disloyalty’, and ‘The Mega Church’. He is considered to be the largest publishing author in Africa, having had his books translated into over 52 languages with more than 40 million copies in print.
Related to Kitabu Cha Mistari Ya Bibilia Ya Kukari
Related ebooks
Kitabu cha Sherehe Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsWakristo:Mabalozi wa Ufalme wa Mungu Maagizo Kuhusu Kuishi kama Mkristo. Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsEneza Huduma Yako Kwa Miujiza na Udhihirishaji wa Roho Mtakatifu Rating: 4 out of 5 stars4/5Ukweli Muhimu Kwa Ajili Ya Waumini Wapya Rating: 3 out of 5 stars3/5Waambie Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsNamna ya Kuomba Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsAnagkazo (Nguvu ya kushurutisha!) Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsKuanzisha Kanisa Rating: 4 out of 5 stars4/5Mguso Mzuri Wa Upako Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsVitengo vya Ujenzi Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsBadilisha Huduma yako ya kiuchungaji Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsNi Jambo Zuri Sana Kumtumikia Bwana Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsNamna Unavyoweza Kuwa na Muda wa Faragha Mzuri na Mungu Kila Siku Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsJinsi ya Kutangua Laana Rating: 5 out of 5 stars5/5Imani Kwa Wale Walioitwa na Kuchaguliwa na Mungu Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsWale wanaokushitaki Rating: 5 out of 5 stars5/5Mapepo Na Jinsi Ya Kukabiliana Nayo Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsWale Wanaojifanyisha Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsKanisa Kubwa Rating: 4 out of 5 stars4/5Wajue Maadui Zako Wasioonekana... Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsWengine... Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsKurudi Nyuma Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsMmoja Wenu Ni Shetani Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsNguzo za Imani Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsHatua Za Kufikia Upako Rating: 5 out of 5 stars5/5Wale Wana ambao ni Hatari Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsWale ambao ni Wajinga Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsRoho Mtakatifu Rating: 5 out of 5 stars5/5Kusamehe Kumerahisishwa Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsMambo ya Kufanya Saa Yako Ikifika Rating: 0 out of 5 stars0 ratings
Reviews for Kitabu Cha Mistari Ya Bibilia Ya Kukari
2 ratings0 reviews
Book preview
Kitabu Cha Mistari Ya Bibilia Ya Kukari - Dag Heward-Mills
The Holy Bible in Kiswahili, Union Version 1994
© Hakinakili 2017 Dag Heward-Mills
Jina la Awali : Bible Memorisation Handbook
Kwa habari zaidi kuhusu Dag Heward-Mills
Kampeni ya Yesu Mponyaji
Andika kwa: evangelist@daghewardmills.org
Tovuti: www.daghewardmills.org
Facebook: Dag Heward-Mills
Twitter: @EvangelistDag
ISBN : 978-1-64135-377-9
Haki zote zimehifadhiwa na sheria ya kimataifa ya hakinakili. Idhini ya maandishi lazima itolewe na mchapaji ili kutumia au kuzalisha sehemu yoyote ya kitabu hiki.
Yaliyomo
Sura ya 1: Kukariri Bibilia ni Nini?
Sura 2: Umuhimu wa Kukariri Biblia
Mwanza
Kutoka
Mambo ya Walawi
Hesabu
Kumbukumbu la Torati
Yoshua
Ruthu
1 Samweli
2 Samweli
1 Wafalme
2 Wafalme
1 Mambo ya Nyakati
2 Mambo ya Nyakati
Ezra
Nehemia
Esta
Ayubu
Zaburi
Mithali
Mhubiri
Wimbo Ulio Bora
Isaya
Yeremia
Maombolezo
Ezekieli
Danieli
Hosea
Yoeli
Amosi
Yona
Mika
Habakuki
Sefanai
Hagai
Zekaria
Malaki
Matayo
Marko
Luka
Yohanna
Matendo Ya Mitume
Warumi
1 Wakorintho
2 Wakorintho
Wagalatia
Waefeso
Wafilipi
Wakolosai
1 Wathesalonike
2 Wathesalonike
1 Timotheo
2 Timotheo
Tito
Filemoni
Waebrania
Yokobo
1 Petro
2 Petro
1 Yohanna
2 Yohanna
3 Yohanna
Yuda
Ufunua wa Yohanna
Sura ya 1
Kukariri Bibilia ni Nini?
Kukariri Bibilia ni msingi mkuu wa huduma kubwa. Leo, watu wengi hawasimamii msingi imara na hivyo basi hawawezi kuzalisha kazi kubwa kwa Mungu hapa duniani.
Kwa kazi ngumu na mtazamo wenye bidii na tabia ya kiunyenyekevu, utaijenga tabia muhimu inayoweza kubeba karama kuu za Mungu. Kupitia kukariri Biblia huduma yako itaenda kwa viwango vya juu viwezekanavyo.
Kukariri Bibilia ni kuikita akilini mistari ya msingi ili uweze kuinukuu pale inapohitajika.
Kuwa Mfuasi wa Kristo
Akawaambia, Nifuateni, nami nitawafanya kuwa wavuvi wa watu.
Mathayo 4:19
Lazima uelewe kwamba lengo ni kukufanya kuwa mfuasi wa kweli wa Yesu kristo aliyekariri maandiko.
Kila siku maishani ni siku ya kukariri andiko kwenye Biblia.
Kila siku maishani ni fursa kubwa ya kujenga tabia nzuri na iliyoboreshwa.
Kila mazungumzo na mtu mwingine ni fursa ya kukariri andiko.
Kila mazugumzo na mwamini mwenzako ni fursa ya kujaribiwa kwenye ujuzi wako wa kukariri.
Katika kurasa zifuatazo, utapata fungu la maandiko ambalo kila Mkristo anategemewa kukariri. Mimi binafsi nimechagua kila mojawapo ya maandiko haya. Maandiko hayajadhamiriwa kwako kwa kurejea tu. Ni kwa ajili ya kukariri! Kuna maandiko mengi utayajua lakini kuna baadhi ya maandiko ambayo unapaswa kuwa tayari kunukuu!
Beba kitabu hiki wakati wote. Uwe tayari kunukuu andiko lolote wakati wowote ule unapoulizwa. Unapokuwa Mkristo kwa miezi kadhaa, lazima uwe tayari kunukuu mojawapo ya maandiko haya. Hakika lazima uwe mtu wa Mungu wa kunukuu Biblia.
Nakutangazia kuwa mfuasi wa Yesu Kristo na mfano mzuri wa huduma kupitia kitabu hiki cha kipekee cha kukariri Biblia!
Sura 2
Umuhimu wa Kukariri Biblia
Mtumishi lazima awe mbeba Neno la Mungu. Lazima awe mtu aliyevikwa kabisa kwa neno la Mungu na utukufu wake. Ndio maana kukariri Biblia ni muhimu kwa kuendeleza huduma.
Hapo mwanzo kulikuwa na Neno. Hii ina maana kwamba neno la Mungu daima litakuwa kwenye msingi wa kila kitu anachokifanya Mungu.
Leo, kuweka akilini maandiko kunapata umuhimu tena kwa sababu Mungu anajenga kanisa lenye utukufu zaidi. Utukufu wa kanisa hili la mwisho litakuwa bora zaidi kuliko utukufu wa kanisa lilioanza kutangaza habari njema za Yesu Kristo. Hii pia inamaanisha kwamba watumishi watakaoinuka, katika siku za mwisho watakuwa wamepakwa mafuta zaidi na wenye utukufu kuliko kabla. Watalijua Neno la Mungu na kulinukuu kwa wepesi!
Je huduma hizi zenye utukufu na makanisa haya yenye utukufu yatazaliwaje na kuumbwa? Biblia iko wazi kwenye hilo. Kupitia Neno la Mungu mtumishi hujengwa na kutayarishwa kwa ajili ya kazi kubwa katika huduma ya Yesu. Yote haya yanahusu maarifa yetu ya maandiko!
Katika 2 Timoteo 3:16-17, tunaona maono yenye nguvu na muhimu ya jinsi ya kuwa mtumishi bora aliyetayari kwa kazi zote nzuri: andiko!
Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki; ili mtu wa Mungu awe kamili, amekamilishwa apate kutenda kila tendo jema.
Kitabu hiki cha Kukariri kinakupa baadi ya maandiko muhimu ambayo unapaswa kuyajua. Ni mkusanyiko wa thamani wa maandiko yote unayopaswa kuyajua. Chukua maandiko yaliyopo kwenye kitabu hiki moyoni mwako kupitia stadi ya kukariri. Kadiri unavyokariri utakuwa umejipa mwenyewe msingi imara kwa ajili ya huduma.
Kuwa kama Yesu Mkombozi wetu! Yesu Kristo alijawa maandiko aliyokariri.