KUZINDUA MCHAKATO WA MAADHIMISHO YA SHEREHE ZA MIAKA 30 YA JUMUIYA YA TAWALA ZA MITAA TANZANIA Jumuiya ya Tawala za Mitaa nchini (ALAT) ilianzishwa rasmi tarehe 13 Disemba 1984 kufuatia kuanzishwa upya kwa mfumo wa Serikali za Mitaa mwaka 1982.Kwa kuzingatia umuhimu na maendeleo yaliyofikiwa katika sekta ya Serikali za Mitaa nchini Mkutano mkuu wa 30 wa Jumuiya uliofanyika jijini Tanga uliazimia kufanya maadhimisho ya kitaifa ya sherehe za miaka 30 ya ALAT na Serikali za Mitaa. Katika kipindi cha miaka 30 Jumuiya pamoja na Serikali za Mitaa nchini zimepata mafanikio mengi ya kujivunia na hivyo wakati tunafikisha miaka 30 kuna kila sababu ya kujivunia, kuonyesha na kuwaeleza wananchi juu ya mafanikio hayo. Baadhi ya mafanikio yanayostahili kutajwa ni pamoja na Kushawishi na kufanikisha utungaji wa Sera ya Kupeleka Madaraka kwa wananchi The Policy Paper on Decentralization by Devolution, Kushawishi na kufanikisha kupandishwa mishahara na marupurupu ya Wakurugenzi na watendaji wengine wa halmashauri ili kulingana watendaji wengine wa Serikali; Kuandaa kitabu cha Kiada cha madiwani (councillors Handbook) na kutoa mafunzo ya madiwani kwa kushirikiana na Shirika la Maendeleo la Ujerumani na Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI; Kushawishi na kutungwa kwa Sheria ya Marekebisho ya Sheria ya Serikali za Mitaa Na. 6 ya Mwaka 1999,Uanzishwaji wa kada ya Maafisa Watendaji wa Kata, Vijiji na Mitaa na kuondokana na Makatibu Watendaji wa Vijiji/Kata, Uanzishwaji wa Sherehe ya Wiki ya Maadhimisho ya Serikali za Mitaa, Kubuni mbinu za kufadhili Mikutano Mikuu ya ALAT Taifa, Kupitisha hatua mbalimbali za Mpango wa Kuijengea Uwezo Jumuiya uofadhiliwa na Ubalozi wa SIDA (ALAT institutional Strengthening Project).
Kubuni na kusimamia Mradi wa Ushirikiano wa miji katika kujenga uchumi
jamii (Municipal Partnership for Local Economic Development- MPED) n.k. Leo tunazindua mchakato wa maadhimisho ya za miaka thelathini ya ALAT na Serikali za Mitaa mchakato ambao utaenda sambamba na utekelezaji wa shughuli mbalimbali zifuatazo zitakazotufikisha katika kilele cha sherehe hizo mwezi April 2014; moja ni shughuli ya kutangaza mafanikio ya ALAT na Serikali za Mitaa kupitia mkanda wa sinema (CD) iliyoandaliwa ili jamii ifahamu mafanikio yaliyopatikana kwa kipindi cha miaka 30 ili kuendelea kujenga hoja kwa wananchi juu ya umuhimu wa kuzitumia Serikali zao za Mitaa katika kuwaletea maendeleo kupitia mipango mbalimbali ikiwa ni pamoja na uimarishaji uchumi kwa jamii (local Economic development). Pili, kuendelea kukusanya taarifa kutoka kwa wanachama juu ya utekelezaji wa mkakati wetu wa kuondoa tatizo la madawati shuleni. Tatu, kufanya maandalizi ya mpango wa kumzawadia meya/ mwenyekiti wa Halmashauri aliyefanya vizuri katika halmashauri yake (mayors Award). Mpango huu utakuwa hatua zifuatazo; uombaji (nomination), kutangaza (announcements), kuwapigia kura wenyeviti/mameya wa Halmashauri na utoaji wa zawadi utakaofanyika wakati wa kilelele cha maadhimisho ya miaka 30 ya ALAT na Serikali za mitaa. Nne; kuendelea kufanya maandalizi ya sherehe za miaka 30 ya ALAT na Serikali za mitaa nchini pamoja na maandalizi ya Mkutano Mkuu. Napenda kuchukua fursa hii kuziomba taasisi, mashirika, wabia wa maendeleo na wadau wa Serikali za Mitaa nchini kujitokeza na kuchukua fursa mbalimbali za kufadhili sherehe hizi zitakazofanyika sambamba na Mkutano Mkuu wa Jumuiya pamoja na mpango wa kuwazawadia Mameya/wenyeviti wa Halmashauri. Nawashukuruni sana kwa kunisikiliza na sasa natoa fursa ya kuuliza maswali. Mwisho
Mwenyeki wa ALAT Taifa na Meya Wa Jiji la Dar es Salaam
Taarifa Ya Kamati Kufuatia Matokeo Ya Ukaguzi Maalum Wa Mdhibiti Na Mkaguzi Mkuu Wa Hesabu Za Serikali Katika Akaunti Ya Tegeta Escrow Iliyokuwa Katika Benki Kuu Ya Tanzania