You are on page 1of 3

First National Bank yazindua mikopo ya nyumba

Dar es Salaam, February 19, 2015: First National


Bank Tanzania imezindua mikopo ya nyumba ya
masharti nafuu ikiwemo muda wa miaka 20 kulipa.
Mikopo hii italeta faraja kubwa kwa mamilioni ya
Watanzania wenye ndoto za kumiliki nyumba.
Meneja wa mauzo wa First National Bank Tanzania,
Emmanuel Mongella akiongea wakati wa uzinduzi
wa huduma hiyo ya FNB Home loans leo jijini Dar es
salaam alisema kuwa benki hiyo sasa imeanza kutoa
mikopo ya nyumba kwa riba nafuu ambazo
zinapangwa kutokana na uhusiano wa mteja na
benki na vilevile uwezo wa kukopesheka.
Wateja wetu watafurahia huduma ya haraka na
kupatiwa mikopo katika muda wa siku tatu. Na
katika miezi mitatu ya kwanza tangu uzinduzi,
wateja wetu hawatalipia gharama za huduma katika
mchakato wa kupata mikopo, alisema. FNB
inaamini kwamba huduma hii itakuwa ni suluhisho
kwa wale wote wanaotafuta mikopo ya muda mrefu
ili kununua nyumba na kukarabati nyumba. Mikopo
hii ya FNB inaweza kulipwa taratibu kwa kipindi cha
miaka 20
Mshauri wa Mikopo ya Nyumba wa FNB, Patricia
Nguma alisema mikopo hiyo itagawanyika katika

makundi manne ambayo ni; Mkopo wa kununua


nyumba (home Purchase loan) Mkopo wa kumalizia
nyumba (Home completion loan), mkopo wa
kuwekeza nyumba na kupata fedha (Home equity
loan) na kuhamisha mkopo toka benki nyingine
(Home switch loan).
Mikopo ya nyumba ya FNB imelenga kuwapa faraja
linapokuja suala la kujenga na kumiliki nyumba na
vilevile kufanya ukarabati wa nyumba. Watu kutoka
maeneo yote ya jamii wanaweza kuomba mikopo hii,
alisema.
FNB ni benki iliyosambaa barani Afrika iliyoanza
kutoa huduma kusini mwa jangwa la Sahara tangu
mwaka 1874. Hivi sasa FNB inapatikana Afrika
Kusini, Namibia, Botswana, Zambia, Mozambique,
Lesotho, Swaziland na Tanzania. Benki hii
imedhamiria kuwa taasisi bora zaidi ya kifedha
barani Afrika.
FNB Tanzania ilifungua milango yake rasmi nchini
Tanzania mnamo Julai 27, 2011. Sinza na Mbagala
ni tawi la 6 na 7 jijini Dar es Salaam; mengine ni
tawi la posta, tawi la maeneo ya viwanda, tawi la
Peninsula, tawi la Kariakoo na tawi la Kimweri. FNB
ina dhumuni kubwa la kuwa mdau muhimu katika
maendeleo ya sekta ya fedha na imepanga kuendelea
kuanzisha huduma zenye ubunifu na utaalamu wa

hali ya juu hapa nchini na hakika FNB inazingatia


kauli mbiu yake isemayo Tukusaidiaje?
Kwa
taarifa
zaidi
tembelea
tovuti
yetu
www.fnbtanzania.co.tz au tuma barua pepe kwenda
info@fnb.co.tz

You might also like