Professional Documents
Culture Documents
26464
Awali ya yote ifahamike kuwa wanafunzi wanaochaguliwa moja kwa moja kujiunga na kidato
cha tano au vyuo vya serikali ni wale wanaotoka shuleni (school candidates) na si watahiniwa wa
kujitegemea (private candidates).
Kadhalika wanafunzi wanaochaguliwa moja kwa moja katika vyuo vya ufundi mfano Dar es
Salaam Institute of Technology (DIT), Arusha Institute of Technology (AIT) na kama hivyo,
huwa na sifa sawa na wale wanaochaguliwa kuijunga na kidato cha tano katika michepuo ya
sayansi. Idadi ya wanafunzi hawa huwa si kubwa sana.
Mwanafunzi aliyefaulu kwa Distiction na Merits ana nafasi kubwa ya kuchaguliwa kuendelea na
masomo ya kidato cha tano au chuo cha ufundi katika shule na vyuo vya serikali. Aidha hata
waliopata Credit na Pass wana nafasi ya kuchaguliwa. Si tukio la kawaida mwanafunzi aliyepata
divisheni F kuchaguliwa kujiunga kidato cha tano au chuo cha ufundi.
Mara nyingi changamoto wanayokuwa nayo wanafunzi waliofaulu kwa viwango vya juu ni aina
ya michepuo na shule za kuendelea nazo. Ni jambo la kawaida kukuta kijana akifaulu masomo
mengi na kisha kusoma mchepuo ambao hana mapenzi nao sana. Hili husababishwa na
mazingira ya ujazaji fomu za michepuo ya kuendelea nayo baada ya kuhitimu masomo. Hutokea
kuwa mchepuo anaoupenda sana ana shaka ya kufanya vizuri na hivyo kuchaguwa michepuo
mingine. Ama kwa upande wa shule, hutegemeana na nafasi, ufaulu wa wanafunzi na idadi ya
wanafunzi walioomba katika Shule husika.
Baadhi ya wanafunzi wanapokosa michepuo au shule walizoomba huhangaika na kutumia muda
mwingi wakitaka kubadilisha. Uzoefu unaonyesha kwamba ni sehemu ndogo za sana ya
wanafunzi hao ambao hufanikiwa. Ushauri wetu ni kwamba endapo kijana atachaguliwa katika
shule asiyoipenda na hakuna sababu za kiafya za kumfanya asiende katika shule hiyo pengine
kutokana na hali ya hewa, au kachaguliwa mchepuo asioupenda na familiya yake haina uwezo
wa kumsomesha shule binafsi, basi atulizane katika hicho alichopata na ajikite zaidi katika
masomo kwani anaweza pia kufanikiwa katika fursa hiyo aliyoipata.
Changamoto nyingine ambayo huwakuta vijana wa kundi hili ni kuanza kusoma tuisheni za
masomo ya kidato cha tano kabla ya uchaguzi kufanyika. Utata wa jambo hili ni kama
tulioueleza hapo juu wa mwanafunzi kuchaguliwa mchepuo tofauti kabisa na masomo
anayosoma. Kwa mfano kuna kijana tunayemfahamu akisoma masomo ya mchepuo wa
Economic, Geography na Mathematics (EGM) lakini akachaguliwa mchepuo wa History, Kiswahili
na Language (HKL). Tofauti iliyoje! Katika hilo inashauriwa kuwa kama mwanafunzi hana hakika
ya kusoma katika shule binafsi, asianze masomo hayo mpaka baada ya uchaguzi wa kidato cha
tano kufanyika. Na ikibidi kujisomea asome vitu vya jumla kama masomo ya lugha, kompyuta
nk.
Kwa wale waliokwisha amua au lazima wasome katika shule binafsi, ni muhimu kufanya utafiti
juu ya ubora wa shule hizo kitaaluma, maadili na stadi nyingine za maisha. Aidha ni muhimu
kufuatilia juu ya kiwango cha ada, muda wa kuchukuwa na kurejesha fomu za maombi, tarehe
26464
26464
Mwanafunzi aliyefeli kabisa na kupata Sifuri (0), hana fursa yoyote katika zote zilizotajwa hapo
juu. Hata hivyo anakuwa amepata cheti cha kuhudhuria masomo (leaving certificate) ambacho
huwa na msaada fulani katika maisha kwa kuna wakati huhitajika vijana waliomaliza kidato cha
nne bila kujali ufaulu wake.
Pia kuna fursa zinazohitaji vijana waliomaliza shule ya msingi ambazo bado zinaweza kutumiwa
na vijana hawa. Kwa mfano kuna fani mbalimbali zinazotolewa na vyuo vya VETA kama ufundi,
udereva, usafi,utunzaji bustani, upishi nk ambazo zinaweza kutumiwa vema na vijana ambao
hawakufaulu mitihani ya kidato cha nne.
Ni muhimu kutaja hapa kwamba si waliofeli tuwanaoweza kuzitumia fursa za mafunzo ya VETA
bali hata wale waliopata divisheni Pass na hata Credit ambao ama hawakupata fursa za
kuchaguliwa kidato cha tano au familiya zao hazimudu kuwasomesha katika shule au vyuo vya
kujilipia.
Kurudia Mitihani
Wanafunzi wengi wanaofanya vibaya katika mitihani yao, jambo la haraka linalowajia vichwani
ni kurudia mitihani. Ndio maana siku hizi vituo vinavyotoa mafunzo kwa wanaorudia mitihani
vimekuwa vikiongezeka kila kukicha. Ni kwakuwa soko linakuwa na wateja wameongezeka.
Pamoja na kuunga mkono na kuheshimu juhudi za wanaotoa mafunzo hayo, tungependa
tutanabahishe kwamba ni ili kuepusha upotevu mwingi wa muda na pesa, ni vema mwanafunzi
akawa akijiandaa kurudia mitihani huku akijufunza ujuzi mwingine. Uzoefu unaonyesha kuna
wanafunzi wanaorudia mitihani na matokeo yao kuwa mabaya kuliko ya mwaka uliotangulia.
Aidha kuna wanafunzi waliorudia mitihani zaidi ya mara moja na bado hawakufanikiwa kupata
alama C au zaidi (credits) tatu walizohitaji ili wajiunge na kidato cha tano.
Endapo mwanafunzi atajiandaa kurudia mitihani huku anapata ujuzi mwingine mfano udereva,
ufundi,nk anakuwa katika nafasi nzuri ya ajira hata asipofaulu mitihani yake anayorudia. Ni
uzuri ulioje endapo atapata vyote - credits na huku ana cheti cha ujuzi wake.
Jambo hili linawezekana endapo kijana ataugawa vizuri muda wake chini ya muongozo wa
familia kwa mfano asubuhi akienda chuoni kupata ujuzi na jioni akienda tuisheni kwa ajili ya
kurudia mitihani. Aidha endapo mwanafunzi hatofanikiwa kupata credits, anaweza kuanza kazi
huku ajiandaa taratibu kurudia mitihani yake. Wengi wamefanikiwa kwa utaratibu huu.
Kukata rufaa juu ya matokeo
Wapo wanafunzi ambao wanakuwa hawakuwa hawakuridhika na matokeo waliyopata wakiamini
hawakutendewa haki katika usahihishaji pengine kwa kuzingatia rekodi za matokeo yao katika
mitihani ya shuleni au kwa jinsi walivyofanya mitihani.
26464
Kwamba hatupingi jambo hili ndivyo pia tungependa kusisitiza kuwa wakati ukikusudia hilo ni
vema ukaendelea na mipango mingine ya kujiendeleza kama tulivyoitaja hapo juu. Hii ni
kwasababu ni wanafunzi wachache sana ambao matokeo yao hubadilika baada ya mitihani yao
kusahihishwa upya. Aidha unaweza kupoteza muda mwingi ukisubiri hatma ya rufaa yako na
kisha majibu kuja usivyotarajia.
Ufadhili wa Masomo
Hutokea wanafunzi waliopata nafasi za masomo katika shule binafsi au vyuo vinavyohitaji
kujilipia wakawa hawana uwezo wa kujisomesha na hivyo kuhangaika huku na kule kutafuta
ufadhili. Ukweli ni kuwa ni wachache sana ambao hufanikiwa. Hii ni kutokana na kutokuwa na
taasisi rasmi zinazotoa ufadhili katika viwango hivi ya elimu nchini.
Pamoja na kutokatishana na tamaa, ni vema mtu unapokuwa katika hali hiyo kutafuta shughuli
itakayokuwezesha kujenga nguvu za kiuchumi na kisha kuweka akiba kwa ajili ya kujisomesha.
Unaweza kuweka malengo ya kusoma huku ukifanya kazi. Endapo shughuli zako hazikupi fursa
ya kusoma huku ukifanya kazi, unaweza kuahirisha kusoma hadi kipindi fulani baada ya
kujiimarisha kiuchumi. Endapo hilo litakuwa gumu kulitekeleza, familia iangalie uwezekano wa
kuuza sehemu ya rasilimali endapo inazo na ambazo hazitaithiri familia nzima endapo zitauzwa.
Tuhitimishe kwa kusema, matokeo vyovyote yawavyo hayawezi kuwa ndio mwisho wa maisha.
Siku zote wanaofanikiwa ni wale wanaotazama mbele huku wakijifunza kwa yaliyowatokea.
Walofaulu washukuru huku wakijipanga; waliofanya vibaya wasubiri huku wakijifuza. Tumia
vizuri kila fursa unayoipata bila kujali udogo wake. Jifunze kwa wengine, uliza, pata miongozo
kwa waliokutangulia, na amini kuwa ipo siku ufanikiwa. Washindi hawaachi, na wenye kuacha
hawashindi.
KUVUNJIKA KWA KOLEO SI MWISHO WA UHUNZI
Kwa Msaada zaidi wa ushauri na namna bora ya kusoma tafadhali wasiliana nasi kwa namba
255 767 488856
au barua pepe marshk86@hotmail.com
26464