Professional Documents
Culture Documents
Wakati Tanzania inajiandaa kuelekea kwenye uchaguzi mkuu wa madiwani, wabunge na raisi
vijembe zimekuwa zikitawala hapa na pale nchini kote. Kama mtanzania mwingine,nimeona
mambo mengi mazuri yamefanyika katika miaka mitano ya awamu ya kwanza ya uongozi wa
kiuchumi, kisiasa na kijamii zilizolikabili taifa letu pendwa, vilevile kumekuwa na tafiti
mbalimbali kupima kukubalika kwa Raisi katika utendaji wake nchini mwetu, matokeo ya tafiti
hizi yalionyesha wananchi wengi kuridhika na utendaji wa Raisi wetu. Kwa kuzingatia matokeo
raisi kunatokana na ufanisi wake binafsi kama kiongozi makini ama ni kwa vile anatekeleza
Mara kwa mara ninapofuatilia utendaji wa Mheshimiwa raisi, na hata ninapokuwa nikisikiliza
hotuba zake katika nyakati tofauti tofauti, ninajivunia kuwa na kiongozi makini ambaye kamwe
haumi maneno, wala kuficha kitu wakati anazungumzia masuala nyeti ya nchi yetu pendwa ya
Tanzania. Kwa uadilifu na umakini wake wakati mwingine naona kuna baadhi ya viongozi ndani
ya CCM wanamungusha kwa kundekeza vitendo vya rushwa, hapo najiuliza, kama kwa kiwango
ambacho Mheshimiwa raisi anakubalika, kwa umakini wa utendaji wake na uhodari wake wa
uongozi, je , Mheshimiwa raisi akisimama kugombea uraisi bila CCM ina maana watanzania
hatutomchagua tena kuwa raisi wetu? Ama ikiwa Mheshimiwa raisi atajiunga na chama tofauti
kiongozi makini alipo bila kujali sana yupo kwenye chama gani. Naamini kiongozi makini katika
Tanzania anaweza kutoka CCM, CUF, UPT-Maendeleo, NCCR,TLP, CHADEMA, SAU ama chama
kingine chochote cha siasa. Katika miaka takribani kumi na nane (18) tangu kuanza rasmi kwa
demokrasia ya vyama vingi, tumeshuhudia viongozi kutoka vyama tofauti vya siasa katika ngazi
za udiwani na ubunge ingawa nafsi ya uraisi imebaki kwa chama cha mapinduzi. Ni wazi
maamuzi wakati wa uchaguzi kama wakati huu. Kuendeleo kukua na kukomaa kwa demokrasia
ya vyama vingi kunahitaji viongozi watoke vyama tofauti tofauti vya siasa kulingana na uwezo
na umakini wao wa kuongoza. Hatuna budi kuwaamini viongozi kutoka vyama vya upinzani ili
waingie bungeni wakachangie sio tu ustawi wa demokrasia bali pia maendeleo ya nchi kwa
kuisimamia serikali, kuikosoa na kuingoza kwa kupitisha miswada makini katika nyanja
mbalimbali.
Ndugu zangu, tungejuaje uwezo wa Zitto Kabwe kama wana wa Kigoma wasingemwamini na
kumpa kura za ndio kuwa mbunge wao? Tungejuwaje Dr Taarabu mbunge wa CUF kuwa ni
kiongozi makini nje ya fani ya Tiba kama wananchi wa jimbo lake wasingempa kura za ndio?
Hata huyu Dr Slaa, mbunge wa Karatu tungejuaje kuwa husoma nyaraka nyeti mara mbili mbili
kabla hajazisaini ikiwa CHADEMA hawakumpa nafasi. Vipi kuhusu Mheshimiwa Magufuri,
Mheshimiwa Ngereja na hata mzee Mizengo Pinda wa CCM, wote hawa wameaminiwa na
kupewa nafasi kwa nyakati tofauti na wengi wetu tumekubali sana ufanisi wao.
Salaam zangu kwa watanzania wenzangu ni tubadili fikra zetu tunapoelekea kuchagua viongozi
watakaoshikilia nafasi nyeti za uongozi nchini mwetu kwa miaka mitano ijayo, nionavyo baadhi
ya watu wameamua kugombea nafasi za uongozi kupitia CCM kwa kuamini kuwa kazi yao ni
kuhakikisha wanafanya fitna na hila ili wapitishwe na vikao halali vya CCM, kwa vile kupitishwa
na vikao halali vya CCM ni tiketi tosha ya kushinda uchaguzi mkuu ujao kiulaini, kwani haipingiki
uwezo na nguvu za CCM katika uchaguzi huwa sio za kitoto, CCM wanajua sana kufanya
kampeni kiasi kwamba hata kama baadhi ya wagombea wa upinzani watashindana na kivuli cha
CCM, sio ajabu kukuta kivuli kinapata kura nyingi zaidi kuliko wapinzani. Matokeo haya ni
kielelezo cha ukongwe wa CCM katika kushinda chaguzi kwa kishindo. Angalizo hapa ni kuwa,
tunapoelekea kupiga kura, tusipumbazike tu na mgombea kuwa katika chama fulani pendwa, ni
vizuri zaidi kuzingatia uwezo wa mgombea katika kusimamia ilani ya uchaguzi ya chama chake,
uwezo na nia yake ya dhati kuwaletea maendeleo wanajimbo wenzake. Itashangaza sana
kuchagua viongozi ambao hawakerwi wala kuumizwa na shida za wapiga kura wao.
Jawabu la Mheshimiwa Raisi Jakaya Kikwete anaihitaji CCM ili kushinda uchaguzi mkuu hapo
Oktoba 2010, ni wazi sio rahisi kusema ndio ama hapana, lakini nionavyo ikiwa Mheshimiwa
Raisi Kikwete akigombea nafasi ya uraisi kwa tiketi ya chama tofauti na CCM, sitoshangaa
kumwona anapoteza nafasi yake ya uraisi. Kwa mtazamo huo hapo ndipo najiuliza mara mbili
mbili, siri ya ushindi ya CCM ni nini? Kwa vile pamoja na kuongoza nchi kwa miaka zaidi ya
thelathini sasa, bado nchi inahangaika na tatizo la maji ya uhakika, achilia mbali ubora wa maji
yanayopatikana, nchi bado inahangaika kuwa na umeme wa uhakika, huduma za afya na elimu
bado sio bora hata kwenye majiji kama Mwanza,Dar es Salaam, Arusha, Mbeya na Tanga achilia
mbali huko kwenye vijiji vingine ndio sababu baadhi ya vijana wa vijijini wanaona ni bora
wakimbilie jijini Dar es Salaam wakafaidi japo kidogo mema ya nchi. Pamoja na hayo, bado CCM
inashinda kwa kishindo kwenye uchaguzi mkuu unaoendeshwa kwa Haki na Huru, hili halina
ubishi. Hivyo, Mheshimiwa Raisi akithubutu kugombea kwa chama kingine tofauti na CCM, hiyo
itakuwa imekula kwake, ni wazi hana wazo hilo kwa vile anaijua sana CCM.
Ikumbukwe, lengo la salaam hizi kwa watanzania wenzangu ni kuwachalenji ili tutafakari kwa
kina mustakabali wa nchi yetu pendwa, na tufanye maamuzi sahihi wakati tunaelekea kwenye
uchaguzi mkuu, silaha zetu mkononi katika kupiga vita rushwa na tamaa ya baadhi ya
viongozi wetu kujilimbikiza mali kwa njia zisizo rasmi ni KURA, tujitokeze kwenye kampeni
matatizo yetu kwa kadri ya mahitaji yetu. Kimsingi kipindi cha kampeni wagombea wanapopita
majimboni kuomba kura ni sawasawa na mtu anapokwenda kwenye usaili wa kazi, hivyo
kampeni hizi tuzitumie kuwauliza maswali ya mambo muhimu ili tuwapime kama wanastahili
hizo ofisi nyeti za umma na kama wana uwezo wa kututumikia vema. Kama ilivyo kwenye usaili,
usipokidhi vigezo vya kazi ni wazi wenye kazi yao hawakupi nafasi , hata kama utalia machozi ya
damu, hivyo tuwape nafasi za uongozi wagombea wetu kwa kuzingatia vigezo na mahitaji yetu.
Ikumbuke kuwa ikiwa hatutopata viongozi makini , maendeleo yatachelewa kwa miaka mingine
mitano. Kwa vile ndoto za kujiletea maendeleo yetu hakuna awezaye kuzitekeleza kama sisi