Professional Documents
Culture Documents
Habari za asubuhi. 1. Napenda kuchukua fursa hii kuwashukuru wote mliofika katika mkutano huu muhimu wenye lengo la kuwaelimisha wananchi na wadau wa Sekta ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) kuhusu umuhimu wa kuundwa kwa Tume ya kitaifa ya kuratibu, kusimamia na kuendeleza TEHAMA nchini. Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) ni moja kati ya Sekta zinazokua kwa kasi hapa nchini na duniani kote na imekuwa ikichangia kikamilifu katika maendeleo ya Taifa na pia imekuwa ikiwezesha sekta nyingine kukua na kuboresha maisha ya wananchi na huduma za jamii kwa ujumla. Kutokana na ukuaji wa Sekta hii, jitihada za makusudi zinahitajika katika kusimamia na kuratibu shughuli za TEHAMA ili nchi iweze kunufaika zaidi kwani mchango wa sekta hii unaweza kuwa mkubwa kama TEHAMA na matumizi yake yataratibiwa, kusimamiwa na kuendelezwa vyema zaidi kuliko hali ilivyo sasa. Katika kuhakikisha masuala ya TEHAMA nchini yanaratibiwa, kusimamiwa na
kuendelezwa vyema, Serikali iliona ni vema ikaundwa Tume ya TEHAMA (ICT Commission). Uamuzi huu pamoja na mambo mengine, unatambuliwa na Sera ya Taifa ya TEHAMA ya mwaka 2003 ambayo pia inaelekeza kuundwa kwa chombo cha TEHAMA ikiwemo juhudi na program mbalimbali zinazoendelea hapa nchini zinazohitaji utaratibu wenye ufanisi. Aidha, Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia inaendelea na taratibu za uanzishwaji wa Tume ya TEHAMA ikiwepo juhudi na program mbalimbali zinazoendelea hapa nchini zinazohitaji uratibu wenye ufanisi. Kwa kutambua mchango wa wadau katika ukuzaji wa sekta ya Mawasiliano nchini, wadau mbalimbali wa masuala ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano wamehusika na kushiriki kikamilifu kutoa maoni katika hatua zote za uanzishwaji wa Tume hii. Tume hii inalenga kutambua na kuvutia fursa za uwekezaji katika TEHAMA, kutoa ushauri, kuendeleza rasilimali watu kitaifa kwenye sekta ya TEHAMA, kuendeleza program za kitaifa za TEHAMA na kushiriki katika kuendeleza miundombinu mbalimbali ya TEHAMA yenye sura ya kitaifa kwa kushirikisha wadau wa sekta zote.
certification) na kuhakikisha utoshelevu wa rasilimali watu utakaokidhi mahitaji ya maendeleo ya TEHAMA; Kutokuwepo chombo mahususi chenye majukumu ya kisheria.