You are on page 1of 2

TUME YA VYUO VIKUU TANZANIA

TAARIFA KWA UMMA

VYUO NA PROGRAMU ZILIVYOZUILIWA KUDAHILI


WANAFUNZI WA MWAKA WA KWANZA KWA MWAKA
WA MASOMO 2017/18

1.0 Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) inapenda kuuarifu umma kuwa,
mwezi Septemba na Oktoba mwaka 2016 ilifanya uhakiki wa vyuo vyote
vya elimu ya juu nchini ili kuhakiki ubora wa elimu inayotolewa vyuoni.
Ripoti ya uhakiki ilionesha mapungufu kadhaa katika baadhi vyuo. Kwa
sababu hiyo, Tume imesitisha udahili wa wanafunzi wa mwaka wa
kwanza kwa mwaka wa masomo 2017/18 kwa vyuo vifuatavyo:
1. Eckenforde Tanga University
2. Jomo Kenyatta University, Arusha
3. Kenyatta University, Arusha
4. United African University of Tanzania
5. International Medical and Technological University (IMTU)
6. University of Bagamoyo
7. St. Francis University College of Health and Allied Sciences
8. Archibishop James University College
9. Archibishop Mihayo University College
10. Cardinal Rugambwa Memorial University College
11. Kampala International University Dsm College
12. Marian University College
13. St. Johns University of Tanzania Msalato Centre
14. St. Johns University of Tanzania, Marks Centre
15. St. Joseph University College of Engineering and Technology
16. Teofilo Kisanji University
17. Teofilo Kisanji University Tabora Centre
18. Tumaini University, Mbeya Centre
19. Kilimanjaro Christian Medical University College (KCMCo)

2.0 Aidha, kutokana na mapungufu katika vyuo mbalimbali imeamriwa


kwamba jumla ya programu 75 kutoka vyuo 22 nchini zimesitishwa
kudahili wanafunzi wa mwaka wa kwanza kwa mwaka wa masomo
2017/18. Kuona Programu ambazo zimesitishwa kudahili wanafunzi kwa
mwaka wa masomo 2017/18 tafadhali bonyeza hapa.

3.0 Aidha Tume inapenda kusisitiza kwamba, uamuzi huu hautawahusu


wanafunzi wanaondelea na masomo katika programu na vyuo husika.

Imetolewa na:

Prof. Eleuther Mwageni


Kaimu Katibu Mtendaji
24 Julai 2017

You might also like