Professional Documents
Culture Documents
Fungu kuu: Yohana 15:13 Hakuna aliye na upendo mwingi kuliko huu, wa mtu
1YOHANA 4:8 Yeye asiyependa, hakumjua Mungu, kwa maana Mungu ni upendo.16.
Nasi tumelifahamu pendo alilo nalo Mungu kwetu sisi, na kuliamini. Mungu ni upendo,
naye akaaye katika pendo, hukaa ndani ya Mungu, na Mungu hukaa ndani yake.
*Tunapaswa kutambuwa kwa kuwa upendo ndiyo asili ya Mungu kila anachofanya ni
upendo, hata sheria yake ni upendo hata ghadhabu yake na hukumu zake ni upendo.
Yohana 3:16 Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe
pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele.
WAEFESO 2: 4 Lakini Mungu, kwa kuwa ni mwingi wa rehema, kwa mapenzi yake makuu
aliyotupenda;5 hata wakati ule tulipokuwa wafu kwa sababu ya makosa yetu; alituhuisha
pamoja na Kristo; yaani, tumeokolewa kwa neema.
TITO 3: 3 Maana hapo zamani sisi nasi tulikuwa hatuna akili, tulikuwa waasi,
tumedanganywa, huku tukitumikia tamaa na anasa za namna nyingi, tukiishi katika uovu
na husuda, tukichukiza na kuchukiana.4 Lakini wema wake Mwokozi wetu Mungu, na
upendo wake kwa wanadamu, ulipofunuliwa, alituokoa;
ROHO YA UNABII :The Desire of Ages / Tumaini la Vizazi Vyote ; Page 6 Chap : God with
us / Mungu pamoja na si
" The earth was dark through misapprehension of God. That the gloomy shadows might be
lightened, that the world might be brought back to God, Satan's deceiptive power was to
be broken. This could not be done by force. the exercise of force is contrary to the
principles of God's Government; He desires only the service of love; and love can not be
commanded; it can not be worn by force or authority; Only Love is Love awakened
" Kwa kuwa ulimwengu haukumjua Mungu, giza nene liliifunika dunia, ili kulimulika na
kuliondoa giza nene na kuirudisha dunia mikononi mwa Bwana, ilibidi kuzivunja hila za
mwovu shetani.
Jambo hilo halikuhitaji matumizi ya nguvu, kwa maana matumizi ya nguvu ni kinyume na
kanuni za serekali ya Mungu; Mungu huridhia huduma ya upendo; na upendo
haushurutishwi; na haupatikani kwa matumisi ya nguvu wala mamlaka; Upendo pekee
huamsha Upendo"
kanuni za Serekali ya Mungu upendo ndio mkuu kuliko kitu chochote sio kama serekali za
dunia zenye kuacha majeraha makubwa na visasi katika mioyo ya wanadamu. Ndiyo
maana japo tupo katika dunia serekali yetu nambari moja inapaswa kuwa ya Mbinguni na
kanuni hiyo ndiyo tuifuate
Yohana 15:13 Hakuna aliye na upendo mwingi kuliko huu, wa mtu kuutoa uhai wake kwa
ajili ya rafiki zake.
Upendo wetu sisi una mapungufu sana" Kisa cha Mwanamume aliedai kumpenda mke
wake na kuitangazia dunia nzima, upendo wake ulipojaribiwa kwa kutoa figo yake
kumuokoa mke wake huyo, akashindwa."
YEREMIA 31: 3 Bwana alinitokea zamani, akisema, Naam nimekupenda kwa upendo wa
milele, ndiyo maana nimekuvuta kwa fadhili zangu.
WAFILIPI 2: 6 ambaye yeye mwanzo alikuwa yuna namna ya Mungu, naye hakuona kule
kuwa sawa na Mungu kuwa ni kitu cha kushikamana nacho;
7 bali alijifanya kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa ana mfano wa
wanadamu;8 tena, alipoonekana ana umbo kama mwanadamu, alijinyenyekeza akawa
mtii hata mauti, naam, mauti ya msalaba.\
RUMI 5: 8 Bali Mungu aonyesha pendo lake yeye mwenyewe kwetu sisi, kwa kuwa Kristo
alikufa kwa ajili yetu, tulipokuwa tungali wenye dhambi.
WEBRANIA 2: 9 ila twamwona yeye aliyefanywa mdogo punde kuliko malaika, yaani,
Yesu, kwa sababu ya maumivu ya mauti, amevikwa taji ya utukufu na heshima, ili kwa
neema ya Mungu aionje mauti kwa ajili ya kila mtu.
Yesu alipokufa pale msalabani haikuwa mauti hii ya usingizi tunayopatwa nayo sisi, kwa
sababu mauti hii ya kwanza haiwezi kuihukumu dhambi, mauti ya pili ndio Mwisho wa
dhambi na wadhambi na hii ndio iliokuwa mauti ya Msalaba Yesu alikua tayari kuangamia
na asiwepo milele ili mimi na wewe tuishi milele!
Ufunuo wa Yohana 2:11 Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho ayaambia
makanisa. Yeye ashindaye hatapatikana na madhara ya mauti ya pili.
Ufunuo wa Yohana 20:6 Huo ndio ufufuo wa kwanza. Heri, na mtakatifu, ni yeye aliye na
sehemu katika ufufuo wa kwanza; juu ya hao mauti ya pili haina nguvu; bali watakuwa
makuhani wa Mungu na wa Kristo, nao watatawala pamoja naye hiyo miaka elfu.
Upendo ndiyo siri ya wokovu wetu, bila upendo isingewezekana kutuokoa dunia imefika
pabaya kwa sababu upendo hatuna upendo.
"God could have destroyed Satan and his sympathizers as easly as one can cast a pebble
to the earth; but he did not do this, rebellion was not be overcome by force. Compelling
power is found only under Satan's government. The lord principles are not of this order.
His Authority rests upon goodness, mercy, and love; and the presentation of this principles
is the means to be used. God government is moral, and truth and love are to be the
prevailing power.
1WAKORINTHO 13:13 Basi, sasa inadumu imani, tumaini, upendo, haya matatu; na
katika hayo lililo kuu ni upendo.
Upendo wetu umepoa : MATHAYO 24:12 Na kwa sababu ya kuongezeka maasi, upendo
wa wengi utapoa.
WITO : Ni wangapi wanasema ewee Bwana Yesu kaa ndani yangu ili uniambukize
upendo wa agape, kama ulivyonipenda mimi nami nimpende Mungu kwa moyo wangu
wote na kwa akili zangu zote na jirani yangu kama nafsi yangu, uniwezeshe kutoa mali
zangu na muda wangu kwa mguso wa upendo wa agape ili kuwasiadia wahitaji.
Yuko mtu ambaye ni kama mimi ambaye anasema nimeusaliti upendo wa Bwana kiasi cha
kufanya maovu yasiyoelezeka, na nataka nizaliwe upya kwa maji (ubatizo) na kwa Roho
(Utakaso) ili nife kwa ubinafsi nifufuke kwa upendo wa Agape, Tembea uungane nami
tusimame mbele za Bwana tumulilie atuokoe.
Bwana Awe nanyi Daima.