Professional Documents
Culture Documents
10 SEPTEMBA 2017
Makusanyo haya ni sawa na ukuaji wa asilimia 1.2 ikilinganishwa na makusanyo ya kipindi kama
hicho kwa mwaka wa fedha 2016/17.
Katika kipindi hicho cha miezi mitatu, makusanyo ya kila mwezi yalikuwa kama ifuatavyo;-
Aidha, Mamlaka inapenda kuwakumbusha wafanyabiashara wote kutoa risiti za kielektroniki kwa
kila mauzo na kudai risiti kwa kila manunuzi kwani ni njia pekee ya kupata mauzo sahihi
yanayoiwezesha TRA kukokotoa kodi sahihi na kwa haki.
Napenda kuwakumbusha wananchi wote kuhakiki risiti zao ili kuona usahihi wa tarehe
na kiasi walicholipa na bidhaa waliyonunua kabla ya kuondoka na risiti hiyo. Endapo
utaona haina vigezo tafadhali ripoti kwenye ofisi ya TRA iliyokaribu nawe au piga simu
kituo chetu cha huduma kwa wateja kwa namba 0800750075 au 0800780078. anasisitiza
Richard Kayombo, Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipakodi
Vile vile, Mamlaka inawakumbusha wamiliki wa majengo nchini kulipa kodi ya majengo mapema
badala ya kusubiri mwishoni mwa mwaka wa fedha ili kuepuka misongamano na usumbufu usio
wa lazima.
Pia, wafanyabiashara wa michezo ya kubahatisha wanapewa wito wa kulipakodi zao kwa mujibu
wa sheria ya michezo ya kubahatisha sura namba 41.