Professional Documents
Culture Documents
Ndugu Wananchi,
Mabibi na Mabwana,
2
Assalamu Aleikum
Katika kipindi hiki cha miaka 54 ya Mapinduzi, tunasherehekea kuwepo kwa hali ya
amani, umoja na maendeleo makubwa yaliyopatikana. Tuna wajibu mkubwa wa
4
kuzichukua mwaka 2011/2012, hivi sasa, utegemezi wa bajeti yetu kwa mwaka
2017/2018, umefikia asilimia 7.3, ikilinganishwa na asilimia 30.2 katika mwaka
2010/2011. Mafanikio haya tuliyopata ni makubwa na ya kupigiwa mfano.
Kasi ya ukuaji wa uchumi wetu kwa bei halisi, imekua kwa asilimia 7.0 kwa mwaka
2017, ikilinganishwa na asilimia 6.8 kwa mwaka 2016. Aidha, Pato la Mtu Binafsi
nalo limeongezeka na kufikia TZS. 1,806,000 ikilinganishwa na TZS 1,632,000 kwa
mwaka 2015. Kasi ya mfumko wa bei ilifikia asilimia 5.6 katika mwaka 2017 kutoka
asilimia 6.7 mwaka 2016. Lengo letu ni kuimarisha uchumi, kupunguza umasikini na
kuifanya Zanzibar kuwa miongoni mwa nchi zenye uchumi wa kiwango cha kati
ifikapo mwaka 2020.
Nawashukuru wakulima wa karafuu kwa kuziuza karafuu zao katika Shirika la ZSTC.
Navipongeza vikosi vya Ulinzi na Usalama na Idara Maalum za SMZ kwa kuyadhibiti
magendo ya karafuu.
Hivi leo, skuli za msingi zimeongezeka mara saba, skuli za sekondari zimeongezeka
mara 53 na idadi ya wanafunzi wa skuli za Msingi na Sekondari imeongezeka mara
14, kutoka wanafunzi 25,372 mwaka 1963 hadi wanafunzi 378,211 mwaka 2017.
Tatizo walilotutengenezea wakoloni kwamba watoto wa wafanyakazi na wakulima
tusiingie sekondari na kupata elimu ya juu, leo halipo tena. Haya ni mafanikio
makubwa ya kupigiwa mfano.
Katika jitihada ya kuongeza madarasa, mwaka 2017, Serikali ilianza ujenzi wa skuli 9
za ghorofa za sekondari kwa Unguja na Pemba, ambapo ujenzi wake, pamoja na
vituo vya mafunzo ya amali kwa Mkoa wa Kusini Unguja na Mkoa wa Kaskazini
Pemba unaendelea. Aidha, ujenzi wa jengo jipya katika Taasisi ya Karume ya
Sayansi na Teknolojia umefikia asimilia 85.
Mipango yetu ya elimu imepata mafanikio makubwa ambapo sasa Zanzibar inavyo
Vyuo Vikuu Vitatu vinavyoendeshwa na wataalamu wetu wenyewe. Kiasi cha
wanafunzi 1,800 wa fani mbali mbali wanahitimu kwenye Vyuo Vikuu vya Zanzibar,
kila mwaka. Kwa hivyo, Zanzibar itajitosheleza kwa kuwa na wataalamu wake
wenyewe hivi karibuni.
Kumalizika kwa Mradi huu kutaongeza upatikanaji wa maji safi na salama kutoka lita
milioni 67 na kufikia lita milioni 81, sawa na ongezeko la asilimia 20.9.
Kuhusu visima 150 vilivyochimbwa katika maeneo mbali mbali ya Unguja na Pemba,
kwa msaada wa Serikali ya Ras Al Khaimah, visima 26 tayari vinatoa maji na
yanatumika na visima 14 viliendelea kutayarishwa, katika mwaka 2017.
Katika mwaka 2018, Serikali inaendeleza utafiti wa mafuta na gesi kwa kutegemea
taarifa itakayotolewa na wataalamu baada ya utafiti uliofanywa. Serikali itatoa taarifa
rasmi kwa wananchi kuhusu matokeo ya utafiti huu unaofanywa kwa maslahi ya
Zanzibar.
Katika mwezi wa Disemba 2017, Serikali iliandaa Sera Mpya ya Ardhi ya Zanzibar,
ambayo itaimarisha utawala na usimamizi wa sekta ya ardhi. Kuandaliwa kwa sera
mpya ya ardhi kutapelekea kufanyiwa marekebisho sheria nane za ardhi za Zanzibar.
Ili kuongeza kasi ya ufanisi na kuongeza tija katika kuiendeleza sekta ya mifugo,
hivi karibuni Serikali imeanzisha Taasisi mpya ya Utafiti wa Mifugo. Katika mwaka
wa fedha, 2017/2018, Taasisi hiyo imepatiwa TZS. milioni 500 ambapo imeanza
kufanya tafiti 6 ikiwemo athari za minyoo katika ng’ombe na matumizi ya mwani
kama chakula cha mifugo. Kadhalika, jumla ya vikundi 18 vya wafugaji vimepatiwa
ng’ombe 368 na mbuzi 720 wa maziwa kwa mpango wa kopa ng’ombe lipa ng’ombe.
Vile vile, vijana 60 wamepatiwa elimu ya huduma za mifugo vijijini, ili kuwasaidia
wananchi katika vijiji vyao.
Ukuu (km. 11.7), kwa kiwango cha lami na bara bara ya Kwarara - Matumaini
zimekamilika na zimezinduliwa rasmi jusi katika sherehe za Mapinduzi. Vile vile,
ujenzi wa Barabara ya Bububu - Mahonda - Mkokotoni (km 31) unatarajiwa kuanza
wakati wowote kuanzia sasa kwa mkopo wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB).
Mjenzi wa barabara hio tayari amekabidhiwa eneo la ujenzi huo.
Kuhusu ujenzi wa bandari mpya ya Mpiga Duri, ujenzi wake utaanza baada suala la
mkopo wa ujenzi huo kufanyiwa kazi na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na hatimae kujadiliana na Benki ya
Exim ya China, kuhusu mkopo huo.
Aidha, huduma za bandari ya Malindi zimeimarishwa kwa kununuliwa vifaa vipya vya
kuchukulia na kupimia makontena pamoja na vifaa vya kukagulia mizigo na abiria
15
Kwa upande wa wastaafu, Serikali imeongeza pensheni kwa viwango mbali mbali.
Vile vile, pensheni jamii iliyoanzishwa na Serikali kwa wazee wote waliofikia umri wa
miaka 70, bila ya kuzingatia kazi walizokuwa wakifanya, imeendelea kutolewa kwa
mafanikio. Jumla ya wazee 27,627 wamelipwa jumla ya TZS bilioni 10.175 tangu
utaratibu huo ulipoanzishwa, mwezi wa Aprili, 2016, ambapo kila mzee analipwa
TZS. 20,000 kwa mwezi.
Katika mwaka 2017, Serikali imeimarisha shughuli za Mahkama katika ngazi mbali
mbali ikiwemo Mahkama ya Ardhi na Mahkama ya Watoto. Hivi sasa kasi ya
usikilizaji wa kesi imeongezeka baada ya Serikali kuongeza idadi ya Majaji na
Mahakimu. Juhudi hizo zitaendelezwa kwa kuyafanyia matengenezo makubwa
majengo ya Mahkama, pamoja na kuanza ujenzi wa jengo jipya la Mahakama Kuu
huko Tunguu. Ujenzi wa Mahkama hio unatarajiwa kuanza hivi karibuni.
Katika mwezi wa Aprili, 2017 Serikali ilitimiza ahadi yake, ambapo ilipandisha
mishahara kwa watumishi wa umma katika ngazi mbali mbali, ikiwa ni mara ya nne
tangu Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Awamu ya Saba ilipoingia madarakani
17
Natumia fursa hii kutoa pongezi zangu kwa Mheshimiwa Dk. John Pombe Joseph
Magufuli katika jitihada zake za kuiongoza Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na
watu wake pamoja na kupambana na vitendo vya rushwa, ufisadi, uhujumu wa
uchumi, dawa za kulevya na kuzilinda raslimali za nchi yetu. Sote ni wajibu wetu
tumuunge mkono katika vita hivi kwa kuzingatia kuwa rushwa ni adui mkubwa wa
haki na ni adui wa jitihada zetu za kuleta maendeleo nchini.
hatua, ili nchi yetu iendelee kupiga hatua kubwa zaidi na ibaki kuwa nchi ya amani
na utulivu.
MAPINDUZI DAIMA